Breaking News
Loading...

TAHARUKI: UGOMVI MKUBWA WAZUKA GWAJIMA VS MAKONDA, MITANDAO YA KIJAMII YACHOCHEA

Share on Google Plus



KUFUATIA sakata la kupambana na madawa ya kulevya na vuguvugu la visa baina ya RC MAKONDA na ASKOFU GWAJIMA..




LEO BAADA YA sauti ya askofu huyo kusambaa katika mitandao ya kijamii ,, kuna ujumbe usio rasmi na kutoka vyanzo visivyo vya kuaminika umekuwa ukienezwa kwa kasi


 Mijadala mingi pia imezuka juu ya hatua ya dhumuni la ujumbe huo wenye DHAMIRA YA KUMCHAFUA RC wengine wakisema ni sawa na inabidi awajibishwe juu ya elimu yake na wengine wakipinga wakisema ni heri kiongozi huyo aachwe afanye kazi yake kwenye kupambana na madawa ya KULEVYA.. Lakini wote hakuna mwenye uhakika juu ya ukweli na uthabiti wa ujumbe huo..  





Ujumbe ni huu.. 

*CV YA PAUL MAKONDA*
1. Alizaliwa tar.15/02/1981 katika kijiji cha Koromije, wilaya ya Misungwi, mkoa wa Mwanza.
2. Majina yake halisi ni *Daudi Albert Bushite*
3.  Alianza darasa la kwanza mwaka 1988  katika shule ya msingi Koromije akitumia majina ya *Daudi Albert Bushite*. Mwaka 1991 alifeli darasa la 4, akarudia. 
4. Mwaka 1992 alifeli tena na hivyo akahamishiwa Mwanza mjini, ili aweze kusoma na kupata masomo ya jioni (tuition).
5. Mwaka 1996 alihitimu darasa la 7 lakini hakuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya serikali.
6. Mwaka 1997 akajiunga na kidato cha kwanza shule ya sekondari ya Pamba.
7. Mwaka 2000 akahitimu kidato cha 4 na kupata daraja sifuri (division zero).
8. Mwaka 2001 akatumia cheti cha Ndg.Paul Christian Muyenge (chenye div.3 ya points 25) kujiunga na chuo cha uvuvi Nyegezi (Nyegezi Fisheries Training Institute) kwa masomo ya Certificate akahitimu mwaka 2002.
9. Mwaka huohuo 2002 akitumia cheti cha *Ndg.Paul Christian Muyenge*, alijiunga na Chuo cha uvuvi Mbegani Bagamoyo kwa masomo ya Diploma ya uvuvi (ORDINARY DIPLOMA IN MASTER FISHERMAN, NTA LEV.6), na kuhitimu mwaka 2005.
10. Mwaka 2003 alikutana na Ndg.Benjamin Sitta (mtoto wa Marehemu Samwel Sitta, ambaye ni Mayor Kinondoni kwa sasa). Wakawa marafiki.
11. Mwaka 2005 baada ya kuhitimu Stashahada yake ya uvuvi, aliomba admission Chuo cha Kilimo Sokoine kusoma shahada lakini akakosa nafasi.
12. Baada ya kukosa nafasi alienda kuishi nyumbani kwa Marehemu Sitta akiwa kama rafiki wa Ben (mtoto wa Sitta). Kwakuwa alitoka familia duni, Sitta aliahidi kumsomesha elimu ya juu.
13. Mwaka 2006, alipata udahili Chuo cha ushirika na biashara Moshi (wakati huo kikiwa chuo kikuu kishiriki cha SUA), kwa kutumia vyeti vyake vya certificate (ya Nyegezi) na diploma (ya Mbegani).
14. Alidahiliwa kwa course ya BA in Cooperate Management &Accounting. Mwaka 2007 alimaliza first year lakini akashindwa kuendelea na 2nd year baada ya kupata Suplementary 6 kati ya Course 8 alizokua akisoma (akawa discontinued).
15. Mwaka huohuo 2007 akaomba Admission upya. Akamaliza first year akiwa na _carries 3_ ambazo alienda nazo 2nd year. Mwaka 2008 akiwa 2nd year akapata supplementary 4 kati ya course 8 alizokua akisoma. Akawa na mzigo wa _carry over_ na _supplementary_. Akaamua kuacha chuo.
16. Mwaka 2008 akaenda kujaribu kuomba udahili chuo kikuu SUA kwa mara nyingine lakini akakosa.
17. Mwaka 2009 akarudi tena MUCcoBS kwa udahili mpya. Akaachana na CMA akachagua Community &Economic Development (CED).
18. Mwaka 20012 akahitimu shahada ya kwanza ya Community &Economic Development kwa jina la *_Paul C Makonda_* badala ya majina yake halisi ya *_Daudi A Bushite_*
19. Jina *_Makonda_* analitumia baada ya kula kiapo mahakamani kubadili jina. Cheti cha Form four kinasomeka *_Paul C Muyenge_* lakini vyeti vya elimu ya juu vinasomeka *_Paul C Makonda_* baada ya kuapa mahakamani.
20. Ndugu Daudi Albert Bushite ameoa (tangu mwaka 2009) lakini hajabahatika kupata mtoto. Na ndiye mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa sasa.


You Might Also Like

0 comments

About me

Like us on Facebook

MICHEZO

Blog Archive