Breaking News
Loading...

MWANAUME UWE NA MSIMAMO KAMA HUU

Share on Google Plus

*MAMA MKWE* 👂🏾


_Ilikuwa wakati wa mchana ambapo mume alirejea nyumbani akiwa na habari mbaya._

*MUME:* _Mpenzi, nimepigiwa simu: Mama hajisikii vizuri. Tunaweza kwenda kumnunulia baadhi ya mahitaji kwa ajili ya kumtembelea?_

```Tafadhali andika orodha ya mahitaji kisha tuondoke.```



*MKE:* _Orodha ya vitu hivyo sio muhimu, tutanunua tu kabichi 2 na lita 2 za mafuta ya kupikia._

*MUME:* _Vitatosha kweli?_

*MKE:* _Ndiyo mpenzi, hakuna haja ya kupoteza pesa, vitatosha._

```Walielekea mjini na kununua kabichi 2 na lita 2 za mafuta ya kupikia. Wakati wakinunua mume alimuuliza mkewe tena kama vitu hivyo vingetosha.```


_Mke alisisitiza zaidi kuwa hawatakiwi kutumia pesa nyingi kwenye ziara ya kushtukiza._

```Walianza safari kuelekea kijijini, na walipofika kwenye eneo la njia panda yenye barabara zinazoelekea vijiji mbalimbali, mume alikata kona kuelekea kwao na mke.```

*MKE:* _(Kwa mshituko) tunaelekea wapi mpenzi? Nilidhani tunaenda kumtembelea mama yako._

*MUME:* _Ndiyo, ndiko tunakuelekea. Ni mama yako (mama yetu) ndiye anayeumwa._

*MKE:* _(kwa mshituko na kilio), lakini mahitaji haya hayatoshi. Turudi tuongeze vitu vingine._

*MUME:* _Hapana! Nilikuuliza tena na tena kama mahitaji hayo yanatosha, ukaniambia “NDIYO”. Hakuna kurudi….._

```FUNZO:```

```Wafanyie wenzako kile unachotaka ufanyiwe!!```

*Yes, hatupendagi ubaguzi sisi.*
🙈🙈🙈‼

You Might Also Like

0 comments

About me

Like us on Facebook

MICHEZO